Muhtasari wa Matokeo ya Kidato cha Sita 2026 NECTA Huu Hapa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) katika Mkutano wake wa 172 uliofanyika tarehe 4 Julai 2026 katika ofisi zake za Mikocheni, Dar es Salaam, liliidhinisha kutangazwa rasmi kwa matokeo ya mitihani iliyofanyika mwezi Mei 2026.
Mitihani Iliyotangazwa
NECTA ilitangaza matokeo ya mitihani ifuatayo:
1. Mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE)
Mtihani wa Advanced Certificate of Secondary Education Examination (ACSEE) kwa watahiniwa wa shule na kujitegemea.
2. Mitihani ya Ualimu kwa Mitaala ya Zamani
- Grade A Teacher’s Certificate Examination (GATCE)
- Diploma in Secondary Education Examination (DSEE)
3. Mitihani ya Ualimu kwa Mitaala Iliyoboreshwa ya 2023
- Diploma in Primary Education Examination (DPEE)
- Diploma in Pre-Primary Education Examination (DPPEE)
- Diploma in Special Education Examination (DSPEE)
Takwimu za Usajili wa ACSEE 2026
Jumla ya watahiniwa 133,647 walijiandikisha kufanya mtihani wa Kidato cha Sita.
- Wanawake: 65,217 (48.80%)
- Wanaume: 68,430 (51.20%)
Kati yao:
- Watahiniwa wa shule: 126,556
- Watahiniwa wa kujitegemea: 7,091
Mahudhurio ya Watahiniwa wa Shule
Kati ya watahiniwa wa shule:
- Waliofanya mtihani: 125,320 (99.02%)
- Hawakufanya mtihani: 1,236 (0.98%)
Kwa jinsia:
- Wanawake waliofanya mtihani: 61,835 (99.12%)
- Wanaume waliofanya mtihani: 63,485 (98.93%)
Mahudhurio ya Watahiniwa wa Kujitegemea
Kati ya watahiniwa 7,091 waliosajiliwa:
- Waliofanya mtihani: 6,476 (91.33%)
- Hawakufanya mtihani: 615 (8.67%)
Takwimu za Mitihani ya Ualimu
GATCE
- Waliosajiliwa: 4
- Waliofanya mtihani: 4
DSEE
- Waliosajiliwa: 1,540
- Waliofanya mtihani: 1,523 (98.90%)
- Hawakufanya mtihani: 17 (1.10%)
DPEE
- Waliosajiliwa: 10,672
- Waliofanya mtihani: 10,427
- Hawakufanya mtihani: 245 (2.30%)
Kwa jinsia:
- Wanawake waliofanya mtihani: 6,720 (98.20%)
- Wanaume waliofanya mtihani: 3,707 (96.81%)
Soma zaidi: NECTA Matokeo ya Mtihani wa Ualimu 2026 DSEE, GATCE, DPEE, DPPEE na DSPEE




Leave a Reply
View Comments